Tangazo

October 30, 2013

Usajili Uhuru Marathon waanza

Katibu wa kamati ya maandalizi yam bio za Uhuru wa Tanzania (Uhuru Marathon ) Bwana Innocent Melleck akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya maandalizi yam bio hizo ambapo fomu za ushiriki zinatarajiwa kuanza kuuzwa rasmi kesho katika vituo 13 jijini Dar Es Salaam na jumanne kwenye viwanja vya bunge mjini Dodoma  ambapo spika Anna Makinda ataongoza wabunge kuchukua fomu za kuishiriki. Kushoto ni mdau wa riadha, Mroki Mroki.


 ***************
Na Mwandishi wetu

USAJILI kwa watu wanaotaka kushiriki mbio ndefu za Uhuru, maarufu kama Uhuru Marathon, zinazotarajiwa kufanyika Desemba 8, mwaka huu jijini Dar es Salaam umeanza rasmi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Kamati ya mbio hizo, Innocent Melleck alisema, mara baada ya Dar es Salaam fomu za usajili zinatarajiwa kutolewa Dodoma kuanzia wiki ijayo.

“Tunapenda kutangaza rasmi kwamba usajili kwa ajili ya mbio hizo umeanza rasmi katika Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo kuna vituo zaidi ya 13 vilivyofunguliwa katika maeneo mbalimbali.

“Pia siku ya Jumanne na Jumatano wiki ijayo fomu hizo zitatolewa rasmi katika Viwanja vya Bunge, Dodoma ambapo Spika Anne Makinda ndiye anayetarajiwa kuongoza katika kujisajili.

“Kingine mtu anayetaka kushiriki anaweza pia kujisali kwa njia ya mtandao wa internet na tunafanya utaratibu maalumu wa kuhakikisha pia yoyote anayetaka anaweza kujisaili kwa njia ya simu, “ alisema.

Melleck alisema, katika usajili huo, fomu zitakazotolewa kwa mshiriki wa kilomita 3 atalipa Sh 100,000 yule wa kilomita 5 Sh 2,000 na washiriki wa kilomita 21 na 42 watalipia Sh 6,000.

“Pia tunapenda kuchukua fursa hii kuziomba kampuni au taasisi mbalimbali zinazotaka kudhamini mbio hizo zijitokeze na kufanya hivyo, kwani nafasi bado ipo na tukumbuke bila amani hakuna chochote kinachoweza kuendelea, hivyo hata wao pia wanatakiwa kuipigania amani kwa nguvu zote.”

Mbio hizo zinatarajiwa kushirikisha wanariadha kadhaa maarufu duniani.

No comments: