Tangazo

March 22, 2014

UCHAGUZI CHALINZE: RIDHIWANI AITEKA KIWANGWA

 Ridhiwani afanya mikutano mitano ya hadhara na miwili zaidi maalum kwa Wazee na Vijana wa Kiwangwa,maeneo ambayo mgombea wa ubunge kupitia CCM alifanya mikutano ya hadhara ni Kijiji cha Msuguru,Mwetemo,Msinune,Bago na Kiwangwa.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambaye pia ndio mratibu wa shughuli za kampeni za ubunge wa jimbo la Chalinze akihutubia umati wa watu waliofurika kwenye uwanja wa kata ya Kiwangwa.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimnadi mgombea wa Ubunge kupitia CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete kwa wananchi wa Kijiji cha Kiwangwa katika jimbo la Chalinze.
Mratibu wa Kampeni za CCM Jimbo la Chalinze Nape Nnauye wakicheza muziki kidogo pamoja na Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM wakati wa kumtambulisha na kumnadi mgombea huyo kwa wapiga kura wa Kiwangwa.
 Mgombea wa Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete akihutubia mamia ya watu waliofurika kwenye mkutano wa kampeni za CCM na kusisitiza tashirikiana nao bega kwa bega katika kuleta maendeleo.
 Umati wa wakazi wa Kiwangwa wakimsikiliza mgombea wa ubunge jimbo la Chalinze kupitia CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa amedhamiria kuinua wananchi wa jimbo hilo kielimu,afya,maji na namna ya kutatua tatizo la wakulima na wafugaji kuwasaidia vijana na kusisitiza kuna umuhimu wa kudumisha michezo kwa jimbo la Chalinze.
 Meneja wa Kampeni za Ubunge jimbo la Chalinze kupitia CCM Ndugu Steven Kazidi akihutubia wakazi wa mji wa Kiwangwa wakati wa mkutano wa hadhara wa kampeni za kumnadi mgombea ubunge kupitia CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete.
 Katibu wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Shaibu Akwilombe akihutubia wakazi wa Kiwangwa wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge kupitia CCM.
 Mtela Mwampamba akihutupia wakazi wa Kiwangwa na kuwaambia mahusiano mazuri kati ya nchi ya Tanzania na CCM ni makubwa mno.
 Msanii Maarufu 'Dokii' akicheza na madansa wake wakati wa mkutano wa kampeni za ubunge  za CCM jimbo la Chalinze .
 Vijana wa Boda Boda wakiongoza msafara wa mgombea wa ubunge CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete kuelekea kwenye mkutano wa hadhara.

 Mgombea wa Ubunge CCM Ndugu Ridhiwani Kikwete akizungumza na Bibi Tanazina Mrisho Mfaume wa kijiji cha Msinune ambapo pamoja na mengi waliyoongea pia Bibi alielezea furaha yake na kuzungumzia CCM inavyoleta maendeleo kwa wananchi wake.

No comments: