Tangazo

April 3, 2014

Wajumbe wengi wa Kamati za Bunge Maalum la Katiba wataka mfumo wa Serikali Mbili

 Na Magreth Kinabo-  Maelezo Dodoma
 
Wajumbe  wengi wa Bunge Maalum la Katiba wamependekeza kuwepo kwa Muundo wa  Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania  wenye mfumo wa  Serikali mbili, wakati wa kuchambua sura ya kwanza na ya sita  zilizoko katika Rasimu ya Katiba mpya.

Hayo yamesemwa leo na wenyeviti wa Kamati namba 10 na moja wa Bunge hilo wakati wakizungumza na waandishi wa habari kwenye Ukumbi  wa mikutano wa St.Gasper mjini Dodoma kwa nyakati tofauti.

 Akizungumzia kuhusu mambo yaliyojiri , Mwenyekiti wa Kamati namba 10 wa  Bunge hilo, Anna Abdalaah  alisema kazi ya kuchambua Rasimu ya Katiba mpya ainaendelea vizuri na  wajumbe wengi wamependekeza mfumo huo huku wakiwa na sababu zao ambazo zitaoneshwa katika ripoti yao.

Alisema Kamati yake ina wajumbe 52, ambapo upande  wa Tanzania Bara una wajumbe 37 na Zanzibar 15.


“Hatuna matatizo ya kutoelewana , kazi inaenda vizuri leo tumemaliza masuala ya shirikisho na muungano ,tumepiga kura hilo halitusumbui, hivi sasa tuko kwenye masuala ya ardhi ,” alisema Mama Anna.

Aliongeza kuwa katika kupitia vipengele vya rasimu hiyo yapo mambo ambayo wote wamekubaliana nayo mfano eneo lote  la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ni eneo lote la Tanganyika  likijumuishasehemu yake ya bahari na eneo lote la Zanzibar likijumuisha  sehemu yake ya bahari , ambapo wameongeza   mito , maziwa, milima na anga.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati namba moja ya Bunge hilo, Ummy Ali Mwalimu alisema katika suala la muundo wa Serikali wengi walitaka suala la Serikali Shirikishi liondolewe, huku  wengi wakisema Ibara ibaki kama ilivyo.

Ummy  aliongeza kuwa wanaendelea na mjadala hadi saa 2:00 usiku, hivyo kesho watapiga kura ili kuweza kumalizia vipengele vingine, hivyo Ijumaa hawataweza kuwasilisha ripoti yao na ameshamwandikia  barua  Mwenyekiti wa Bunge hilo, kuhusu suala hilo.

Naye  Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo,alisema bila kutaja upande upi alisema ukigawa upande mmojakatika 2/3 unapata 12 na mwingine saba, ambapo ikiongeza mtu mmoja  unapata 2/3

 Naye Mwenyekiti wa Kamati namba moja Profesa Makame Mbarawa, Anna Kilango Malecela, ambaye Kamati yake ina wajumbe 53, Tanzania Bara 35 na Zanzibar 18  akizungumza kwa njia ya simu  kwa waandishi wa habari,alisema  wajumbe wote wanataka muungano, hivyo hakuna aliyesema hataki muungano.

Aidha  Kilango alisema wapo baadhi ya wajumbe walitaka serikali mbili na wengine tatu, hivyo wamepisha kuhusu muundo wa Serikali uweje, hivyo wataendelea kupiga kura jioni.

No comments: