Tangazo

June 28, 2014

Kongamano la Mwaka la Maadili ya Waandishi wa Habari na Mkutano Mkuu wa 17 wa Wanachama wa MCT

Rais wa Baraza la habari Tanzania (MCT), Jaji mstaafu Dk. Robert Kisanga akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano la Mwaka la Maadili ya Waandishi wa Habari lililoenda sambamba na Mkutano Mkuu wa 17 wa Wanachama wa MCT, lililofanyika katika eneo litakalokuwa Makao Makuu ya Baraza Kimalang’ombe wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani Juni 24 – 25 mwaka huu. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga, Makamu wa Rais wa MCT, Chande Omar (wa pili kushoto) na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo (DAS), John Mahali. PICHA ZOTE/JOHN BADI wa Daily Mitikasi Blog

Sehemu ya wanahabari na wanachama wa MCT waliohudhuria kongamano hilo.

Mwezeshaji Rosemary Mwakitwange (kulia), akiendesha mjadala elekezi kuhusu changamoto za mfumo huria wa habari, uzoefu wa vyombo vya habari kujisimamia: Kabla na sasana changamoto za vyombo huria:  Kuigawa Nchi/Kuimarisha Demokrasia wakati wa kongamano hilo. Kutoka (kushoto) ni watoa mada, Prof. Mlama, Ndimara Tegambwage na Jenerali Ulimwengu.

Mwanachama wa MCT, Simon Mkina akigawa karatasi za kupigia kura katikauchaguzi wa Rais, Makamu wa Rais na Wajumbe wa Bodi ya MCT, wakati wa mkutano mkuu wa 17 wa wanachama.

Upigaji wa Kura ukiendelea.

Rais wa MCT anayemaliza muda wake, Jaji Mstaafu Dk. Robert Kisanga akipanda mti ndani ya eneo la yatakapokuwa makao makuu ya MCT mjini Bagamoyo. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga na (kulia), Makamu wa Rais wa MCT anayemaliza muda wake, Chande Omar.
XXXXXXXXXXXXXXXXXX

Na John Badi
Daily Mitikasi Blog
Bagamoyo

MKUTANO Mkuu wa 17 wa Wanachama wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), umemchagua Jaji mstaafu Thomas Bashite Mihayo kuwa Rais mpya wa baraza hilo, baada ya aliyekuwa Rais Jaji mstaafu Dk. Robert Kisanga kumaliza muda wake.

Mkutano huo, ulioenda sambamba na Kongamano la Mwaka la Maadili ya Waandishi wa habari ulifanyika katika eneo yatakapo kuwa makao makuu ya baraza hilo, Kimalang’ombe wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani juni 24 na 25 mwaka huu.

Aidha katika uchaguzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC), Hassan Abdallah Mitawi alichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Baraza hilo.

Wajumbe wa Bodi waliochaguliwa kutoka kundi la jamii ni pamoja na Mkuu wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa cha UDSM, Prof. Bernadetha Killian, jaji Mstaafu wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Juston Mlay na Mhandisi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na Mfanyabiashara maarufu Bw. Ali Mufuruki.

Wajumbe wa Bodi waliochaguliwa kutoka Tasnia ya Habari ni pamoja na Rose Mwalimu Haji, Tuma Abdallah kutoka Shirika la Magazeti ya Serikali (TSN), Mkuu wa Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud na  Mhariri Mtendaji wa Gazeti la The Guardian, Warrace Maugo.

No comments: