Tangazo

January 27, 2015

KINANA ATINGA JIMBO LA MTAMBWE ALIKOZALIWA MAALIM SEIF SHARRIF HAMAD WA CUF, AZINDUA MIRADI YA UMEME NA MAJI

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akiweka kifaa cha umeme kwenye transfoma wakati wa uzinduzi wa uwekaji nguzo za umeme katika Kijiji cha Chanjaani, Jimbo la Mtambwe, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, Zanzibar leo. Jimbo hilo ndilo alikozaliwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalimu Seif Sharrif Hamad.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akiweka kifaa cha umeme kwenye transfoma wakati wa uzinduzi wa uwekaji nguzo za umeme katika Kijiji cha Chanjaani, Jimbo la Mtambwe, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba, wakati wa ziara ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya Uchaguzi ya CCM, Zanzibar leo. Jimbo hilo ndilo alikozaliwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad.PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutano wa halmashauri Kuu ya Wilaya ya Wete, ambapo alisomewa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Mkoa wa Kaskazini Pemba na wilaya hiyo.

 Kinana akipata maelezo kuhusu zao la karafuu alipokwenda  kuona ununuzi wa Karafuu katika Ghala la Serikali la ZSTC, wilayani Wete leo.Kushoto ni Mkulima wa zao hilo na Issa Hassan ambaye ni Meneja Utawala wa ZSTC.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akishiriki ujenzi wa Jengo la Ofisi za CCM Tawi la Bopwe, mjini Wete.
 Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinaa akishiriki kupaka rangi majiko ya Mseredani (majiko ya mkaa yanayotengenezwa kwa udongo) katika kikundi cha vijana Jimbo la Gando, wilayani Wete.

 Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana ukielekea Jimbo la Mtambwe kwa kutumia barabara ya kisasa iliyojengwa na Selikali katika Jimbo hilo alilozaliwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad. Katika jimbo hilo Kinana alizindua pia mradi wa utandazaji wa bomba lamji na usimikaji wa nguzo za umeme.
Kinana akiwa na viongozi wengine wa CCM wakifukia mabomba ya maji safi wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Jimbo la Mtambwe, wilayani Wete.

 Kinana akimsikiliza Mwenyekiti wa Maskani ya Chekea  iliyopewa jina na Dk, Jakaya Kikwete katika Jimbo la Mtambwe ambapo vijana wa CUF 35 wamehamia CCM. Vijana hao walidai wameamua kuhamia CCM baada ya kuchoshwa na ahadi hewa za viongozi zikiwemo za Maalim Seif Sharrif Hamad. Pia wameahidi kuwashawishi vijana wengine wa CUF kujiunga na CCM.
 Vijana wa Mtamwe wakishangilia baada ya Mbunge wa CCM Viti Maalumu, kuwaahidi mbele ya Kinana kuwa atawapatia jezi seti mbili kwa ajili ya mchezo wa soka.
 Kinana akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi walipowasili kwenye Chuo cha Ualimu cha Benjamini Mkapa kuzungumza na Serikali ya wanafunzi wa chuo hicho.
 Mtoto wa Hayati Abeid Amani Karume, Ali, akihutubia wananchi mjini Wete ambapo aliwaomba kuipigia kura ya ndiyo Katiba Inayopendekezwa Aprili 30, mwaka huu kwani ina mambo mengi yenye manufaa kwa wazanzibar
 Naibu Katibu Mkuu wa Uoja wa Vijana wa CCM, Shaka, akihutubia katika mkutano huo wa hadhara .
 Wafuasi wa CCM wakicheza kwa furaha katika mkutano huo
Komredi Kinana akihutubia katika mkutano huo
 Sehemu ya umati wa wananchi uliohudhuria mkutano huo uliofanyika eneo la Mtemani, Mjini Wete.



No comments: