Tangazo

October 5, 2011

KAMERA YA DAILY MITIKASI BLOGU KATIKA SOKO LA SAMAKI LA KIMATAIFA LA MAGOGONI MAARUFU KAMA 'FERI' JIJINI DAR KWA NYAKATI TOFAUTI

Siku ukitembelea Soko la samaki la Kimataifa la Magogoni maarufu kama Feri lililopo jijini Dar es Salaam na maeneo yanayolizunguka utajionea mambo mengi sana mengine mazuri na mengine ya kustajabisha kama vile kamera ya Blogu yako ya Daily Mitikasi ilivyoamua kuwaletea mtiririko wa baadhi tu ya taswira za matukio mbalimbali yaliyonaswa katika siku tofauti. Pichani waweza kuona kule ni jambo la kawaida tu mwingine akienda haja ndogo huku mwingine akiosha sandoz zake na wakati huo wengine wakiosha samaki zao basi ili mradi tu.
Siku nyingine kitoweo cha samaki huadimika kutokana na hali ya hewa kuchafuka baharini basi huwa zinasimama hali inayopelekea watu kuuchapa usingizi tu.
Siku nyingine mambo huwa mazuri.
Waweza kukuta kundi kubwa la vijana kama hawa ukadhani eti labda wanapaa samaki, la hasha hawa ni vijana wanaoendekeza matumizi ya bangi na dawa za kulevya... hapo unapowaona kila mtu anasokota kama ni bangi haya weee kama ni unga haya wee...
na wakati mwingine mambo huwa mswano......
lakini pia pembezoni mwa soko hilo huwezi kuwakosa wachapa usingizi katika ufukwe wa bahari ya Hindi wenye upepo mwanana... masaa yooote wao ni usingi tuuuu...
Kinamama wajasiriamali hawakosekani... kama hawa wakipaa samaki baada ya kuwanunua kwenye mnada na kisha huwakaanga tayari kwa kwenda kuwauza reja reja mitaani yaani 'Uswazi'
haya hapo mimi sisimulii kitu utaja mwenyewe...
we mama nunua samaki mimi najisevia pweza huku...
Miundombinu ya Soko la kukaangia samaki bado ni utata kwani moshi unawumiza sana wafanyabiashara wa humo.
Feri hakuna mambo ya Barber Shop... eti sijui niweke Black, ooh mara Magic ooh eti Scrab sijui la hasha kule ni kipara cha wembe kwa kwenda mbele...

No comments: