Tangazo

November 30, 2012

AIRTEL Tanzania kumpongeza Balozi wake AY katika Bonge la Party ndani ya Nyumbani Lounge

Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde na Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo flava) kwa pamoja wakionyesha tuzo ya  Channel 'O'  aliyoipata Mwanamuzi huyo nchini Afrika Kusini. Tukio hilo limefanyika leo wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo Airtel imempongeza AY kwa ushindi alioupa pamoja na kumwandalia sherehe ya kumpongeza itakayofanyika leo usiku nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam.

Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde akiongea wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo Airtel imempongeza AY balozi wake kwa kupata tuzo ya chanel O ya video bora, Katikati ni AY  akifatiwa na DJ wake Athur Baraka.

 Msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongo flava)  na Balozi wa Ambwene Yessaya 'AY' akiwashukuru watanzania kwa kumpigia kura na kumwezesha kupata tuzo hiyo kulia ni Afisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde na kushoto ni  DJ wake Athur Baraka.
****************
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel wakiwa na balozi wake Ambwene Yessaya “AY” leo wamewashukuru watanzania kwa kumpigia kura msaani maarufu wa kizazi kipya Ambwene Yessaya  “ AY “  na kumwezesha kuibuka mshindi wa tuzo ya kwanza katika kipengele cha Most Gifted East African video of the Year kupitia kibao chake kipya kijulikanacho kama “   I don’t wanna be alone”

Akiongea na wandishi wa habari katika Ofisi za Airtel leo AY amechukua fulsa kuwashukuru watanzania kwa kumpigia kura na kuweza kumwezesha kuibuka na ushindi. Aidha alivishukuru vyombo vya habari kwa kuendelea kushirikiana naye katika kufikisha habari na kumsaidia kupata tuzo hiyo.

Naye Afisa uhusino wa Airtel Jane Matinde alisema” tunafurahi kuona msanii AY ambaye ni balozi wetu kuibuka na tuzo iliyoshirikisha wasanii mbalimbali toka  Afrika, sisi tunasikia furaha kuona mafanikio ya wasanii wetu nchini yakiendelea kukua na ndio sababu leo tuko hapa kusherehekea ushindi  huu kwa pamoja na kuwashukuru watanzania kwa kumuwezesha AY kupata tuzo hii kwa kura zenu.

Tunapenda pia kuchukua fulsa hii kuwaalika watanzani na wateja wetu leo pale nyumbani lounge usiku kuanzi saa tatu tuweze kujumuika na AY na kumpongeza kupata tuzo hii. Tutakuwa na wasanii wengi pamoja na wadau mbalimbali wa Musiki na pia utapata muda kupiga picha na msanii huyo na Tuzo yake

MKUTANO MKUU WA NAMANGA SPORTS CLUB KUFANYIKA DESEMBA 09 NDEGE BEACH

Mwenyekiti wa Namanga Sports Club, David Mwaka akiongoza kikao cha maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa Klabu, kilichofanyika Leecar's Pub Namanga jijini Dar es Salaam. PICHA/JOHN BADI
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

- KONYAGI yaupiga 'Jeki'

Na John Badi
 
Mkutano Mkuu Maalum wa Klabu ya Namanga Sports unatarajiwa kufanyika Desemba 09, mwaka huu katika Ukumbi wa Ndege Beach uliopo katika eneo la Mbweni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kikao cha maandalizi, Mwenyekiti wa Namanga Sports Club, Bw. David Mwaka alisema tayari makampuni kadhaa yameshajitokeza kudhamini mkutano huo.

Bw. Mwaka aliyataja makampuni hayo kuwa ni pamoja na Tanzania Distilleries Ltd watengenezaji wa kinywaji maarufu cha Konyagi, Mike Commercial, Esoshi General Trading Co. Ltd na Mele DJ Co. Ltd ya Dodoma.

"Tunawashukuru sana wadhamini ambao tayari wamekwisha onyesha moyo wa kutusaidia, lakini pia tunawaomba wadhamini wengine wajitokeze zaidi ili tuweze kufanikisha mkutano wetu", alisema Bw. Mwaka.

Aidha Bw. Mwaka alitoa wito kwa wanachama wa klabu hiyo ambao bado hawajatoa michango yao ya 20,000/- kuiwasilisha mara moja kwa watu waliopewa majukumu ya kukusanya ambao ni John Gako, Bebee Mangi na Chale JJ.

Wadau wa Takwimu wakutana jijini Dar

Mkurugenzi wa Takwimu nchini, Morrice Oyuke (pichani) akisoma hotuba ya kumwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa  TAKWIMU nchini Dr. Albina Chuwa ( hayupo pichani) katika kongamano la pili la mwaka la wadau wa TAKWIMU nchini jijini Dar es Salaam. PICHA ZOTE/ MWANAKOMBO JUMAA WA MAELEZO

Sehemu ya washiriki  wa kongamano hilo. 

Mwakilishi kutoka Benki ya Dunia, Thomas Danielewitz akitoa hotuba yake.

Naibu wa Wizara ya Fedha, Dk. Saada M. Salum akifungua kongamano hilo.

Sehemu ya washiriki  wa kongamano hilo. 

SIKU YA UKIMWI DUNIANI : WAKAZI WA JIJI LA DAR WAASWA KUPIMA AFYA ZAO NA KUJIKINGA NA UGONJWA WA UKIMWI

Afisa habari wa mkoa wa Dar es salaam Bi. Adrofina Ndyeikiza akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo kuhusu maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani ambayo kimkoa yatafanyika katika uwanja wa Biafra, Manispaa ya Kinondoni. Kulia ni Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Dar es salaa kutoka TACAIDS Bw. Omary Chambo.

Mratibu wa Ukimwi wa Mkoa wa Dar es salaa kutoka TACAIDS Bw. Omary Chambo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kuhusu hali ya maabukizi ya ugonjwa huo katika jiji la Dar es salaam na kutoa wito kwa wakazi wa jiji hilo kushirikiana na serikali na wadau mbalimbali katika kupambana na Ugonjwa huo. Picha na Aron Msigwa - MAELEZO

NAFASI ZA KAZI LEO NOVEMBA 30.2012

Jumbo Operator
African Barrick Gold
DEADLINE : Dec 6, 2012, 12:57:00 PM

Gold Plant Engineering Superintendent
African Barrick Gold
DEADLINE : Dec 14, 2012, 11:12:00 AM

Alimak Superintendent
African Barrick Gold
DEADLINE : Dec 6, 2012, 10:03:00 AM

CCTV Security Coordinator
African Barrick Gold
DEADLINE : Dec 5, 2012, 5:59:00 PM

Program Officers (2 posts)
The Benjamin William Mkapa HIV/AIDSFoundation (BMAF)
DEADLINE: Friday 14th December 2012

Construction Management Officer
The Benjamin William Mkapa HIV/AIDSFoundation (BMAF)
DEADLINE: Friday 14th December 2012

Public Health Specialist (Laboratory/Molecular Biologist)
US Embassy
DEADLINE: December 12, 2012

Electrician
US Embassy
DEADLINE: December 12, 2012

Reservation and Ticketing Sales Agent
Precision Air
DEADLINE : 5th December 2012.

General Manager (1 POST)
Enrich Africa
DEADLINE : 15-12-2012

Hr Manager(1 POST)
Enrich Africa
DEADLINE : 15-12-2012

Finance Manager(1 POST)
Enrich Africa
DEADLINE : 15-12-2012

Operations Manager (1 POST)
Enrich Africa
DEADLINE : 15-12-2012

Branch Manager(3 POSTS)
Enrich Africa
DEADLINE : 15-12-2012

Civil/Mechanical Draughtsman(2 POSTS)
Enrich Africa
DEADLINE : 15-12-2012

Fresher Marketing Graduates(15 Posts)
Enrich Africa
DEADLINE : 30-11-2012

Kwa matangazo ya kazi moja kwa moja kwenye account yako ya facebook like facebook yetu kwa ku-click
HAPA

Mfumo bora wa ufuatialiaji na utoaji wa fedha utatoa motisha kwa uhifadhi na usimamizi endelevu katika sekta ya misitu kwa nchi maskini

Mkurugenzi Ofisi ya Makamu wa Rais,  Mazingira, Bw. Julius Ningu akifuatilia majadiliano ya moja ya nikutano inayoendelea mjini Doha katika mkutano wa 18 wa dunia wa nchi wanachama wa mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi. PICHA/EVELYN MKOKOI
********************
Na Evelyn Mkokoi
Doha

Utoaji wa fedha kwa ajili ya utekelezaji ya kupunguza hewa ukaa na uharibifu wa misitu (MKUHUMI) ulenge kunufaisha wananchi na nchi katika  maeneo husika

Tanzania imesema kuwa, mfumo wa utoaji fedha kwa ajili ya kupunguza utoaji wa gesijoto na uharibifu katika sekta ya misitu hususan kwa nchi zinazoendelea unatakiwa uwe wenye manufaa kwa nchi na wananchi katika maeneo husika.

Hayo yameelezwa leo na Bwana Freddy K. Manyika, Afisa Misitu Mkuu, Ofisi ya Makamu wa Rais, katika majadiliano kuhusu Mfumo wa Ufuatialia na Utaratibu wa utoaji wa fedha, yanayoendelea katika  mkutano wa 18  wa nchi wananchama wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchia unaofanyika mjini Doha, Qatar.

Akiwasilisha msimamo huo wa Tanzania, bw. Manyika ameleeza kuwa,Kuwepo kwa mfumo bora na wa ufuatialiaji na utoaji wa fedha utatoa motisha kwa uhifadhi na usimamizi endelevu katika sekta ya misitu kwa nchi maskini..

Akizungumza kwa niaba ya nchi zinazoendela (Least developed Countries -LDCs) Bw. Manyika alisema kuwa maisha ya wananchi katika nchi zinazoendelea husuan nchi maskini yanategemea sekta ya misitu kwa ajili ya kupata nishati, chakula, madawa, ujenzi wa makaazi na miundombinu, malisho ya mifugo, shughuli za kitamaduni, utalii, na huduma mbalimbali za kijamii kwa kiwango kikubwa, hivyo kwa kuzingatia umuhimu huo, mfumo wa ufuatilaiji na utaratibu wa malipo unaoandaliwa kwa ajili ya kusaidia sekta ya misitu hauna budi kutoa malipo yenye manufaa na motisha kwa wananchi wanaotunza misitu badala ya kutaka kutoa mwanya kwa makampuni ya kibiashara yenye mitaji mikubwa kunufaika na rasilimali hiyo.

 “Tanzania na nchi zinazoendelea hazikubaliani na mfumo unaolenga kuwafanya wananchi wanaozungukwa na kutunza misitu hiyo kwa miaka mingi kugeuzwa vibarua na wapakazi katika makampuni yenye lengo la kujinufaisha kwa kutumia rasilimali na nguvu za wananchi maskini, Alisisitiza.”

Aidha Bw. Manyika aliongeza kuwa, kufikiwa kwa makubaliano kuhusu mfumo na utaratibu wa utoaji wa fedha kwa ajili ya shughuli za MKUHUMI katika mkutano wa Doha utasaidia kurejesha motisha kwa wananchi kuhifadhi misitu katika maeneo yao na hivyo kuendeleza shughuli za utunzaji mazingira na kuchochea maendeleo na uhifadhi endelevu kupitia sekta ya misitu.

Katika majadiliano yanayoendelea hapa mjini Doha, nchi wanachama wanatakiwa kuandaa mfumo wa ufuatiliaji na utaratibu wa utoaji wa fedha kwa shughuli za upunguzaji wa gesijoto na utunzaji wa misitu ili kupunguza uharibifu. Mkutano wa 18 wa nchi wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Mabadiliko ya Tabianchi unafanyika Doha, Qatar, kuanzia tarehe 26 Novemba hadi 7 Desemba 2012.

BOB CHORA AMNG'ARISHA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE'



Msanii wa Sanaa ya Uchoraji, Jeremia Makimata 'Bob Chora' akichora moja ya bango la kumuhamasisha bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' kwa ajili ya mpambano wake unaokuja dhidi ya Bondia Saidi Mundi wa Tanga utakaofanyika Desemba 09, katika Ukumbi wa P.T.A Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Watu wa Marekani washirikiana na Watanzania katika vita dhidi ya VVU/UKIMWI

Ambassador Alfonso Lenhardt launching the "Get Back to Treatment" campaign with Iringa Regional Commissioner Dr. Christine Ishengoma in September. Launched in Iringa in September 2012 and sponsored by the American People, the goal of the campaign was to reach out to and find the missing People Living with HIV(PLHIV) who had stopped treatment and bring those patients back to treatment.  (Photo courtesy of Robert Kiata of Omni Studios)
*****************
Na Balozi Alfonso E. Lenhardt

Tarehe 1 Disemba ya kila mwaka, jumuiya ya kimataifa huadhimisha siku ya UKIMWI duniani. Hii ni siku ya kutafakari kuhusu maisha yaliyopotea, na maisha yaliyobadilika milele kutokana na UKIMWI. Siku hii inatupa fursa ya kuwakumbuka zaidi ya watu milioni 34 wanaoishi na VVU duniani kote. Hali kadhalika, leo tunaadhimisha maisha yaliyookolewa na kuboreshwa nchini Tanzania na kukazia dhamira yetu ya kupambana na UKIMWI.

Aidha, tunatambua maendeleo makubwa yaliyofikiwa duniani katika kipindi cha miaka 30 iliyopita kutokana na tafiti mbalimbali na mbinu za kisayansi zinazotumika katika mapambano haya. Tarehe 23 Julai 2012, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bibi. Clinton alitangaza kuwa Mpango wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kukabiliana na UKIMWI (PEPFAR) utaandaa mpango utakaoainisha awamu ijayo ya ushiriki wa Marekani katika jitihada za kimataifa za kukabiliana na UKIMWI. "Kwa upande wetu, mpango wa PEPFAR utaendelea kuwa kitovu cha utekelezaji wa azma yetu ya dhati ya kuona kuwa tunakuwa na kizazi kisicho na UKIMWI … Tungependa bunge letu lijalo la Congress, Waziri wetu wa Mambo ya Nje ajaye na wabia wetu wote wa hapa nyumbani na kote duniani wapate picha ya mambo yote tuliyojifunza na mpango utakaoonyesha mchango wetu katika kufikia azma ya kuwa na kizazi kisicho na UKIMWI,” alisema Bibi Clinton. 

Mojawapo kati ya mambo tuliyojifunza ni kwamba sote tuna wajibu wa kushughulikia  masuala ya kimataifa yanayohusu afya  na kwamba hakuna nchi yoyote inayoweza kupambana na UKIMWI peke yake. Ili kufanikiwa katika mapambano hayo ni muhimu kwa nchi kufanya kazi na wabia kama vile PEPFAR na mashirika ya kimataifa kama  Mfuko wa Kimataifa wa Kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Global Fund). Kwa pamoja PEPFAR na Global Fund ziliwasaidia zaidi ya asilimia 70 ya watu wote walio katika matibabu ya kupunguza makali ya VVU/UKIMWI katika nchi zinazoendelea katika mwaka 2011.

Hapa Tanzania, ni lazima tuendelee kushirikiana katika kuongeza jitihada zetu dhidi ya VVU na UKIMWI. Kila mmoja wetu -- viongozi wa serikali, sekta binafsi, mashirika ya kimataifa, mashirika ya kiraia na mashirika ya kidini -- ana wajibu katika jitihada hizi. Hatua ya kuiwezesha nchi yenyewe kuchukua uongozi wa programu za kukabiliana na VVU/UKIMWI ni muhimu sana katika kuhakikisha uendelevu wa programu hizo. 
 
Kwa kupitia PEPFAR, Marekani itafanya kazi kwa karibu na Tanzania katika kujenga uwezo wake wa kuongoza, kutekeleza na hatimaye kubeba gharama zote za mapambano dhidi ya UKIMWI kwa kutumia fedha kutoka serikalini, mashirika huru ya kiraia na sekta binafsi ya Tanzania.  Hii inaoana na Azimio la Abuja la Mwaka 2001 linalozitaka nchi wananchama wa Umoja wa Afrika kutenga angalau asilimia 15 ya bajeti zao za taifa kwa ajili ya sekta ya afya. Marekani imedhamiria kwa dhati kuendeleza ushirikiano wake na Tanzania inapoelekea katika kufikia azma hii.

Katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, Tanzania imepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya UKIMWI na Marekani ikiwa na fahari kubwa kusaidia jitihada hizo. Hivi sasa Marekani, kwa kupitia PEPFAR inatoa msaada wa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI kwa zaidi ya watu 364,000 - wanaume, wanawake na watoto. 
 
Katika mwaka wa fedha 2012 pekee, PEPFAR kwa kupitia programu mbalimbali za utoaji matibabu, matunzo na ushauri nasaha iliweza kuwasaidia zaidi ya watu milioni 1.2 nchini Tanzania wakiwemo watoto yatima na walio katika mazingira magumu zaidi ya 526,000. Aidha, programu hizo zimewawezesha akinamama wajawazito milioni 1.1 kupata huduma  ya upimaji wa VVU na ushauri nasaha kwa lengo la kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Mafanikio haya yanayodhihirishwa na maisha ya mamilioni ya watu yaliyookolewa ni makubwa, hata hivyo bado kuna kazi kubwa mbele yetu. Tunatumia maendeleo ya sayansi ili kuhakikisha kuwa tunatumia rasilimali tulizonazo kwa ufanisi na tija zaidi ili tuweze kupata matokeo makubwa zaidi na hivyo kuokoa maisha ya watu wengi zaidi.  Mathalan, tafiti zinaonyesha kuwa tohara kwa wanaume inaweza kupunguza uwezekano wa maambukizi ya VVU kwa wanaume kwa zaidi ya asilimia 60. 
 
Kutokana na hali hiyo, PEPFAR katika miaka mitatu iliyopita imeongeza mara nane mchango wake katika programu ya kuhamasisha tohara ya hiari kwa wanaume nchini Tanzania. Eneo lingine muhimu ni lile la kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto ambapo PEPFAR imeweza kusaidia kutolewa kwa dawa za kuzuia maambukizi hayo kwa karibu asilimia 90 ya wanawake wajawazito waliobainika kuwa na VVU jambo ambalo limeweza kulinda afya ya mama na mtoto.

Tunapoangalia mbele, Marekani itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Tanzania na wabia wake ili kuwa na mipango na shughuli za muda mrefu za kukabiliana na janga hili zitakazookoa maisha ya watu wengi zaidi. Katika kuadhimisha siku hii ya UKIMWI duniani, watu wa Marekani wanathibitisha tena dhamira yao ya dhati ya kushirikiana na Watanzania katika kufikia maono ya pamoja ya kuwa na Tanzania isiyo na VVU.
 ______________________________________________________________________________
Alfonso E. Lenhardt ni Balozi wa Marekani katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

******************************************************************************************
American People Partner with Tanzanians Against HIV/AIDS
 
By Ambassador Alfonso E. Lenhardt

Every year on December 1, the global community commemorates World AIDS Day.  It is a day to reflect on lives lost, and lives forever changed, as a result of AIDS.  It is also an opportunity to pay tribute to more than 34 million people living with HIV worldwide.  Today, we celebrate those lives saved and improved in Tanzania and recommit to the fight against AIDS.

We also acknowledge the tremendous progress the world has made in the last 30 years through research and scientific innovations in this fight. On July 23, 2012 United States Secretary of State Clinton announced that the United States President's Plan For Emergency AIDS Relief (PEPFAR) would deliver a blueprint for the next phase of U.S. efforts on global AIDS “For our part, PEPFAR will remain at the center of America’s commitment to an AIDS-free generation… We want the next Congress, the next Secretary of State, and all of our partners here at home and around the world to have a clear picture of everything we’ve learned and a roadmap that shows what we will contribute to achieving an AIDS-free generation.” 

One of our lessons learned is that global health is a shared responsibility and that no country can fight AIDS alone. To succeed, it is essential that countries work together with partners such as PEPFAR and multilateral organizations like the Global Fund to Fight AIDS, Tuberculosis and Malaria. Together, PEPFAR and the Global Fund supported over 70% of all persons on antiretroviral treatment in developing countries worldwide in 2011.

Here in Tanzania, we must continue to work together to increase our efforts in the response to HIV and AIDS.  Everyone -- government leadership, the private sector, multilateral organizations, civil society, and faith-based organizations -- has a role to play. Progress toward country leadership of HIV/AIDS programs is essential for gains to be sustainable in the long term. Through PEPFAR, the United States is working closely with Tanzania to build the country’s capacity to lead, implement, and eventually pay wholly for its AIDS response with funding from the Tanzanian government, civil society and the private sector.  This coincides with the 2001 Abuja Declaration in which African Union countries pledged to increase government funding for health to at least 15% of the national budget. The United States is committed to our partnership with Tanzania as it moves in this direction.

Over the last 12 months, Tanzania has made good progress in the fight against AIDS, with the United States proud to play a supporting role. In Tanzania, the United States through PEPFAR is currently supporting life-saving antiretroviral treatment for over 364,000 men, women and children.  In fiscal year 2012 alone, PEPFAR directly supported more than 1.2 million people in Tanzania with care and support programs, including more than 526,000 orphans and vulnerable children. Also, its efforts around prevention of mother-to-child transmission programs have allowed more than 1.1 million pregnant women to be reached with HIV testing and counseling.

This progress, evidenced by millions of lives saved, is remarkable, but there is more to do.  We are using scientific advances to focus our resources as effectively and efficiently as possible and to maximize the impact of our investments and save more lives.  For example, studies have shown that male circumcision can diminish acquisition of HIV for men by over 60%.  Therefore PEPFAR has increased its contribution to voluntary medical male circumcision in Tanzania eight-fold over the last three years.  Prevention of mother-to-child transmission is another significant area of focus, whereby PEPFAR support has succeeded in providing prophylaxis to almost 90% of pregnant women identified as HIV-positive - protecting the health of both the mother and her child.

As we look to the future, the United States will continue to work closely with Tanzania and its partners to move toward a long-term response that saves even more lives. On this World AIDS Day, the American people reaffirm our partnership with Tanzanians in our common vision to work towards a Tanzania free of HIV.
______________________________________________________________________________
Alfonso E. Lenhardt is the Ambassador of the United States of America to the United Republic of Tanzania

"KWA TANZANIA YENYE NEEMA... INAWEZEKANA..."

Hawa ni wanafunzi wa moja ya shule zetu za msingi hapa nchini....!

SEND OFF PARTY YA DORICE ALOYCE TENDEWA

 Biharusi mtarajiwa Bi. Dorice Aloyce Tendewa akiwa katika pozi meza kuu wakati wa tafrija maalum ya kumuaga na kumtakia kila la heri katika maisha yake mapya ya ndoa ambayo anataraji kuifunga Jumamosi ya Desemba 1, 2012 katika Kanis la KKKT Usharika wa Azania Front jijini Dar es Salaam. Tafrija hiyo iliyofana sana ilifanyika katika ukumbi wa New Msasani Beach Club.
 Bi. Dorice Tendewa, Biharusi mtarajiwa (kushoto) akiwa na msimamizi wake na rafiki yake mkubwa, Betha Mwakapenda wakati wa tafrija yao maalum ya kumuaga. Production: MD Digital Company +255 755 373999/ 717 002303.
 
 Bi.Dorice Tendewa akisaidiana na Msimamizi wake, Bi. Betha Mwakapenda kukata keki.
  Bi Harusi Mtarajiwa Dorice Tendewa akitambulisha wageni mbalimbali ndugu zake kwa wageni waliofika katika tafrija yake
Picha ya pamoja ya familia nzima ya Bwana na Bibi Aloyce Tendewa. KWA PICHA ZAIDI BOFYA FATHER KIDEVU BLOG

RAIS KIKWETE AKUTANA NA MWENYEKITI WA KANU GIDEON MOI JIJINI NAIROBI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa chama cha KANU Mhe Gideon Moi aliyemtembelea leo Novemba 29, 2012 katika hoteli ya Nairobi Serena jijini Nairobi.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza  Mwenyekiti wa chama cha KANU Mhe Gideon Moi aliyemtembelea na kufanya naye mazungumzo leo Novemba 29, 2012 katika hoteli ya Nairobi Serena jijini Nairobi. PICHA NA IKULU

WAHU KUPAMBA UZINDUZI WA DHANA YA 'WELLNESS' JUMAPILI HII UBUNGO PLAZA

Umewahi kulisikia hili neno?

Kwa ufupi linasanifu dhana nzima ya AFYA.

Ila afya hii inaweza kuwa ya kimwili (physical), kiakili (mental), kipesa (financial), kinahusiano (relationship), kijamii (social), kikazi(occupational), kiroho (spiritual), kihisia (emotional), kimazingira (environmental) na hata ya kitabibu (medical).

Tunahitaji afya zote hizi kuwa kamili na wenye furaha (for optimal well-being).

Dhana hii ya WELLNESS itaelezewa kwa ufupi kwa nini ni muhimu kwako katika hotel wa Blue Pearl, Ubungo Plaza, jumapili tarehe 2 Desemba 2012 toka saa 8 mchana hadi 1 jioni. Wataalam wenye uzoefu katika fani hii watakuelimisha kwa muda mchache.

Uzinduzi huu utasindikizwa na mwanamuziki WAHU KAGWI toka Kenya akikuambia BETTER DAY. “Whatever you are going through today, there always gonna be a better day”.

Kiingilio: 20,000/= only per head

COME ONE, COME ALL.

Tickets zitapatikana 8020 fashions Sinza, maduka yote ya Mariedo ambayo ni IPS, Benjamini Mkapa Towers na Namanga , mlimani city Shear Illusions na Milepamba shop Mwenge Bus stop.

NB: HAKUNA TIKETI ZITAKAZOUZWA MLANGONI SIKU YA JUMAPILI. Deadline Jumamosi saa 4 asubuhi. Only limited seats

NB: Get ready to step on GREEN CARPET for pictures, the carpet of HEALTH

U.S. Embassy Public Affairs Officer (PAO) meets Association of Women in Tourism Tanzania (AWOTTA) leaders

U.S. Embassy Public Affairs Officer Ms. Dana Banks (2nd right) met with the leaders of the Association of Women in Tourism Tanzania (AWOTTA), Ms. Scholastica Ponera (right), Ms. Mary Kalikawe (3rd right) and Ms. Agnes Rwegasira (second left) and U.S. Embassy Alumni Coordinator, Ms. Rehema Kalinga (left) at the U.S. Embassy in Dar es Salaam at the weekend.  AWOTTA's goal is to strengthen women's roles promoting development in Tanzania's tourism sector.  Ms. Banks lauded the association's commitment to promote women leaders in Tanzania's tourism sector to promote economic development. PHOTO/COURTESY OF AMERICAN EMBASSY

DESIGNERS LINE UP FOR TANZANIA RED RIBBON FASHION GALA 2012

Organiser of Tanzania Red ribbon Fashion Gala Ms.Khadija Mwanamboka (second from right) at the group photo with some of the designers at her Office.

Founder and Chairperson of Tanzania Mitindo House (TMH) Ms. Khadija Mwanamboka together with the Kids from the Tanzania Mitindo House Orphanage Centre.

“My Dream is to be a top designer” One of the Orphan get trained for free at Tanzania Mitindo House Office.

DESIGNERS AND MODELS – FIRST ROUND

MOROGORO POLYTEX - VITENGE

1. EVE COLLECTIONS

a)Ava

2. SALIM ALI

a) Ben

3. MARTIN KADINDA

a) Alexia

4. EDNA SILVER

a) Nadia

5. GABRIEL MOLLEL

a) Hidaya

6. SHELLINA IBRAHIM

a) Neema

7. FRANKOO DESIGNS

a) Elgiver

8. Hameed

a) Victor

9. ASIA IDARIOUS KHAMSIN

a) Jamila

TANZANIA RED RIBBON FASHION GALA 2012

FASHION SHOW – SECOND ROUND

DESIGNERS AND MODELS

1. MUSTAFA HASSANALI

a) Jamila

b) Elgiver

c) Alexia

2. Hameed Abdul

a) Ben

b) Hidaya

3.SHELLINA IBRAHIM

a) Neema

b) Jamila

4.GABRIEL MOLLEL

a) Nadya

b) Ava

5.EDNA SILVER

a) Neema

b) Ben

7.EVE COLLECTIONS

a)Ava

b) Hidaya

6. SALIM ALLY

a)Neema

b)Victor

8. MARTIN KADINDA

a) Nadia

b) Alexia

9.FRANKO DESIGNS

a)Ben

b)Victor

10.ASIA IDARIOUS KHAMSIN

a) Elgiver

b)Jamila

EAC SUMMIT NAIROBI

 President Jakaya Kikwete (front, right) met with the Acting Secretary of United States Department of Commerce Dr. Rebecca Blank, (front, left).  Also pictured are United States Ambassador to Tanzania Alfonso E. Lenhardt, (2nd, Left);  Assistant Secretary of Commerce for Market Access and Compliance, Michael Camuñez;  Economic Officer Patrick Collins from the U. S. Embassy in Dar es Salaam Tanzania, and Tanzania Minister of East African Cooperation, Samuel Sitta (2nd, right), during the East African Community (EAC) Summit 2012 in Nairobi, Kenya last week.

 President Kikwete and Acting Secretary of United States Department of Commerce Dr. Rebecca Blank discussed increasing engagement between the United States and East African Community during the EAC Summit 2012 which took place in Nairobi, Kenya on November 28 and 29. PHOTO/COURTESY OF AMERICAN EMBASSY

November 29, 2012

SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WATAALAM WA KUREKEBISHA UPEO WA MACHO KUONA

Dk. Hussein Mwinyi
- Pia yakabidhi Magari tisa na Pikipiki 107 kusaidia huduma za Afya

 Na Aron Msigwa –MAELEZO

Dar es salaam.

Serikali imezindua rasmi baraza la wataalam wa kurekebisha upeo wa macho kuona nchini kwa lengo la kusimamia, kudhibiti na kuratibu utoaji wa huduma bora za macho nchini litakalofanya kazi zake kwa mujibu wa sheria ya Optometria Na.12 ya mwaka 2007.

Akizindua baraza hilo lenye wajumbe 12 leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi amesema kuwa baraza hilo lina wajibu wa kuhakikisha kuwa huduma bora za macho zinaendelea kutolewa kwa kuzingatia taratibu na viwango vilivyowekwa pia kuzingatia umuhimu wa macho katika mwili wa binadamu.

Amesema maisha ya kila siku ya binadamu yanategemea uono wa macho na kuongeza kuwa hali ya kutoona inasababisha maisha ya mwanadamu kuwa hatarini na wakati mwingine kupoteza nguvu kazi ya taifa na kurudisha nyuma maendeleo ya taifa.

"Kila mmoja wetu anafahamu umuhimu wa macho kikiwa kiungo muhimu sana katika mwili wa binadamu kama vilivyo viungo vingine na tusipoona kutokana na matatizo ya macho maisha yetu yanakuwa hatarini".

Amefafanua kuwa baraza hilo lina wajibu wa kuhakikisha kuwa watoa huduma na wapokea huduma wanakua na uhusiano mzuri na kulitaka baraza hilo kutoa elimu ya afya ya macho kwa wananchi juu ya namna ya kutunza macho yao kabla ya madhara kutokea.

Dkt. Mwinyi amesema licha ya Tanzania kukabiliwa na changamoto ya uhaba wa wataalam wa macho serikali inaendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa huduma za macho zinawafikia wananchi wengi hasa maeneo ya vijijini.

Amelitaka baraza hilo kuweka mikakati ya kukabiliana na biashara holela ya miwani isiyokidhi viwango iliyoenea hapa nchini kwa kushirikiana na Halmashauri za manispaa ili kuondoa hatari inayoweza kulikumba taifa kutokana na kutumia miwani isiyokidhi viwango.

"Hivi sasa biashara ya miwani inayouzwa na wamachinga imeenea kila mahali nchini, jambo hili ni hatari kwa afya ya macho kwa watanzania nafahamu linatokana na utandawazi uliokithiri lakini ninyi kama baraza lazima mtafute mbinu ya kukabiliana nalo" amesisitiza.

Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza hilo Bw. Adam Simbeye amesema kuwa baraza hilo jipya linachukua nafasi ya baraza lililozinduliwa mwaka 2009 na kudumu kwa muda wa miaka 3.

Amesema pamoja na mambo mengine baraza hilo katika kipindi cha miaka 3 limefanikiwa kujenga na kulinda maadili ya watumishi wa fani hiyo, kulinda na kudhibiti vituo vya kutolea huduna, kufanikisha zoezi la kusajili vituo vya kutolea huduma nchini na kuhamasisha utii na ufuataji wa kanuni na taratibu za taaluma.

Aidha amesema kuwa baraza linakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa fedha na kukosa ofisi maalum ya kuendesha majukumu yake, aidha amesema baraza hilo limeshindwa kusimamia suala la wafanyabisahara ndogo ndogo (wamachinga) kuuza miwani holela mitaani.

Kwa upande wake mjumbe wa baraza hilo Bw. Anamringi Macha akizungumza kwa niaba ya wajumbe wenzake amesema kuwa uzinduzi wa baraza hilo unawapa nguvu kisheria kutekeleza majukumu yake kwa kipindi cha miaka 3.

Amesema watafanya kazi kwa uadilifu kwa lengo la kuhakikisha kuwa watanzania wote wanapata huduma bora za macho kwa mujibu wa kanuni tarattibu na viwango vilivyowekwa.

"Kuzinduliwa kwa baraza hili kunatupa nguvu kisheria kusimamia, kudhibiti na kuhakikisha huduma za macho nchini zinatolewa kwa viwango na kwa kuzingatia kanuni na taratibu na hili ndilo jukumu letu kuhakikisha maisha na afya za watanzania zinakua salama" Amesema.

Wakati huo huo serikali kwa kushirikiana na shirika la UNFPA, Mfuko wa Dunia na serikali ya Uholanzi imekabidhi magari 9 ya kubebea wagonjwa na pikipiki 107 kwa ajili ya kurahisisha huduma za ukusanyaji wa taarifa za afya, kusafirisha wagonjwa na kuboresha huduma za afya ya mama na mtoto katika maeneo mbalimbali nchini.

Akikabidhi magari hayo kwa wawakilishi wa hospitali zilizopewa magari na pikipiki hizo Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hussein Mwinyi amesema magari na pikipiki hizo yamegharimu fedha nyingi na kuwataka viongozi ambao maeneo yao yamepewa vifaa hivyo kuvitunza ili vidumu na kuendelea kutoa huduma husika.

" Vifaa vilivyo katika magari haya vinatakiwa kutunzwa ili visiharibike au kuibwa ni muhimu sana kukabidhiana kwa maandishi kila inapotokea watumishi wanabadilishana zamu za kutoa huduma katika magari haya" amesisitiza Dkt. Mwinyi.

Amesema magari yenye vifaa vyote yamegharimu shilingi milioni 250 kila moja na yatapelekwa kutoa huduma ya kubebea wagonjwa katika Taassisi ya Mifupa nchini (MOI), Hospitali ya KCMC ,Hospitali za wilaya ya Maswa, Hospitali ya mama Maria wa Kanisa na wilayani Longido.

Aidha amesema magari mengine yatapelekwa katika vituo vya afya wilayani Kahama na Bukombe na kuongeza kuwa baadhi ya pikipiki zilizonunuliwa tayari zimepelekwa katika halmashauri 26 nchini.

Pia amesema kuwa katika kuhakikisha kuwa wagonjwa wanaobebwa katika magari hayo wanakuwa salama hata kama hali zao ni mbaya wizara kwa kutumia wataalam wake imeandaa orodha ya vifaa vinavyotakiwa kuwemo katika gari linalotumiwa kubeba wagonjwa na kusambaza orodha ya vifaa hivyo kwa wadau husiDk. Hussein Mwinyi

Ole Naiko wins Lifetime Achievement Award

ABG's Director of Government Relations, Mr Emmanuel Ole Naiko (left), receives the 2012 Lifetime Achievement Award for Outstanding Public Service from the chairman of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt), Mr Ali Mufuruki.

ABG's Director of Government Relations, Mr Emmanuel Ole Naiko (left), chats with the Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Mr. Peniel Lymo (right), and other officials at a ceremony in Dar es Salaam recently to present Mr Ole Naiko with the 2012 Lifetime Achievement Award for Outstanding Public Service.

ABG's Director of Government Relations, Mr Emmanuel Ole Naiko (left), speaks tp journalists shortly after receiving the 2012 Lifetime Achievement Award for Outstanding Public Service from the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt).

ABG's Director of Government Relations, Mr Emmanuel Ole Naiko (left), poses for a souvenir photograph with the Permanent Secretary in the Prime Minister's Office, Mr. Peniel Lymo (centre), and the chairman of the CEO Roundtable of Tanzania (CEOrt), Mr Ali Mufuruki (right), at a ceremony in Dar es Salaam recently to present Mr Ole Naiko with the 2012 Lifetime Achievement Award for Outstanding Public Service.

FAMILY SPORTS DAY

For More Information Call: +255 755 574 557

November 28, 2012

UZINDUZI WA JENGO LA OFISI ZA JUMUIYA YA AFRIKA YA MASHARIKI

Rais Jakaya Kiwete, Rais wa Kenya, Mwai Kibaki  (wapili kulia) na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza wakivuta kamba kuashiria ufunguzi wajengo jipya la makao makuu ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki mjini Arusha Novemba 28,2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Prince Karim Aga Khan  katika sherehe za uzinduzi  wa jengo la Ofisi Kuu ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki Mjini Arusha Novemba 28,2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiagana Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro,baada ya  sherehe za uzinduzi wa jengo la O(fisi kuu za Jumuiya ya Afrika Mashariki mjini Arusha Novemba 28, 2012. (Picha na Ofisi  ya Waziri Mkuu)

NAPE AONGOZA MAELFU MAZISHI YA SHARO MILIONEA, MUHEZA

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimpa pole  Zaina Mkieli, Mama wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi kwenye mazishi ya msanii huyo, leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga. (Picha na Bashir Nkoromo).

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (Watatu kulia, waliobeba jeneza) akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi, kwenye mazishi ya msanii huyo, leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga. (picha na Bashir Nkoromo)

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa pole za Chama Cha Mapinduzi (CCM) alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga. (Picha na Bashirb Nkoromo).

Baadhi ya wasanii wa muziki wa bongo fleva na filam Tanzania, wakiwa kwenye mazishi ya Sharo milionea.

Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu Tanzania, Hussein Ramadhani, maarufu Saharo Milionea, likiwasili nyumbani kwao, Lusanga, Muheza mkoani Tanga, wakati wa mazishi leo. (Picha na Bashir Nkoromo)

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa na Rais wa Bongo Movies Simon Mwakifyamba na Ofisa Habari wa Airtel Jackson Mbando, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga. (Picha na Bashir Nkoromo).

Mkuu wa wilaya ya Muheza, Subra Mgalu akisoma salam za Shirika la Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) la Mama  Anna Mkapa, kwenye msiba huo. Pamoja naye ni Nape.

Mwana FA akitoa salam kwa niaba ya Wanamuziki wa Bongofleva, wakati wa mazishi hayo.

Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nauye, akitupa mchanga kaburini, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga. (Picha na Bashirb Nkoromo).
Mzee King Majuto akitupa mchanga kaburini kumzika Sharo Milionea.

Ofisa Habari wa Airtel, Jackson Mbando akiwa na  baadhi ya wasanii kwenye mazishi hayo.

Waombolezaji wakimsaidia mwenzao aliyepoteza fahamu msibani, wakati wa mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu Tanzania, yaliyofanyika leo, kijijini kwa marehemu, Lusanga, Muheza mkoani  Tanga.(Picha na Bashir Nkoromo).

Vijana wakiwa wamepanda  mnazi kuona mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga. (Picha na Bashir Nkoromo).